06/02/2025
FALSAFA ZA KUBOJA
2025B KATIKA MTINDO WA SHAIRI
UWAJIBIKAJI
1. Ukitaka pesa, jasho lazima litiririke,
Usitafute njia, za ujanja na hila,
Wajibu ukitimiza, mali itakufuata,
Maisha yatang’ara, utapiga hatua.
2. Kazi si mateso, ni daraja la mafanikio,
Lazima uthubutu, usikae na wasiwasi,
Kupata bila jasho, ni ndoto ya mchana,
Hakuna mafanikio, yasiyo na juhudi.
3. Jitume mapema, kwa moyo wa dhati,
Usingoje kesho, leo ndiyo wakati,
Uzembe na uvivu, vitakuacha maskini,
Mchakato wa maendeleo, huanza na wewe.
4. Pesa si bahati, ni matokeo ya kazi,
Ukitumia akili, utajijenga upya,
Utajiri si mzaha, huja kwa mpangilio,
Wajibu wako ni kuweka juhudi.
5. Fursa zipo tele, jichunguze vizuri,
Anayeamka mapema, hupata anachotaka,
Muda ni mali, usiupoteze bure,
Yeyote anayechakarika, hupata faraja.
6. Jishughulishe sana, uvune faida,
Matumizi makini, ni siri ya tajiri,
Akiba na uwekezaji, visiachwe nyuma,
Kesho hujengwa, kwa misingi ya leo.
7. Elimu ni silaha, itakufaa sana,
K**a unataka pesa, usiache kujifunza,
Maarifa huleta njia, za mapato mapya,
Ukitumia vyema, utafanikiwa.
8. Ushirikiano pia, huleta maendeleo,
Usipende ubinafsi, utakwama njiani,
Kushirikiana na wengine, kunakuza fikra,
Kila mtu ana mchango, katika ustawi wako.
9. Matumizi ya hovyo, ni adui wa pesa,
Hifadhi kile unacho, kilishe kwa hekima,
Usikimbilie anasa, kabla hujajijenga,
Maendeleo ni hatua, hayaji kwa ghafla.
10. Deni lisilo lazima, jiepushe nalo,
Heshimu pato lako, utapiga hatua,
Wajibu wako ni kuweka akiba,
Ili kesho isije, ikakulemea.
11. Bidii ni nguzo, usiache kuitumia,
Kazi yoyote halali, ni baraka kuu,
Tajiri wa kesho, hujengwa leo,
Usingoje muujiza, anza sasa.
12. Ikiwa ni biashara, iweke kwenye msingi,
Uwe na nidhamu, upate faida,
Usikimbilie haraka, ukajutia,
Subira huleta matunda mema.
13. Jitunze afya yako, ndio mtaji mkuu,
Mgonjwa hana nguvu, ya kufanya kazi,
Wajibu wako ni kula vizuri,
Ili mwili uwe na nguvu za kujituma.
14. Heshima kazini, huleta heshima,
Mwajiri atakuthamini, ukijitoa kweli,
Uaminifu ni silaha, ya kupanda juu,
Asiye na uadilifu, hushuka haraka.
15. Wekeza kwa maarifa, sio kwenye starehe,
Fedha itakutumikia, ukijua kuitunza,
Lakini ukiwa mzembe, itakutoroka,
Na utaachwa ukijuta kwa kutokuwa makini.
16. Usiishi kwa mashindano, bali kwa mpango,
Kila mtu na safari yake, jipe muda,
Usijilinganishe na wengine ovyo,
Maendeleo ni yako, yafanikishe taratibu.
17. Pesa mfukoni, huja na nidhamu,
Usitumie hovyo, fanya mahesabu,
Matumizi ya busara, hujenga utajiri,
Na kukuza maendeleo maishani mwako.
18. Mipango thabiti, ni siri ya mafanikio,
Kila shilingi yako, iwe na kazi yake,
Usitumie bila mpango, utajuta baadaye,
Heshimu pesa, itakuheshimu pia.
19. Kila mtu anaweza, ikiwa atajituma,
Hakuna aliyezaliwa, kuwa maskini,
Wajibu wako ni kufanya juhudi,
Maisha mazuri hujengwa na kazi.
20. Hatimaye fahamu, kwamba maendeleo,
Hayaji kwa bahati, bali kwa kujituma,
Usiogope kazi, itakuletea baraka,
Jitahidi leo, kesho itakuwa bora!
Na
KUBOJA
+255(0)656340320
+255(0)763740320
BARIKIWA